Mji wa Tehran utakuwa mwenyeji wa mkutano wa Pendekezo la amani la Hormuz unaotarajiwa kufanyika mwezi ujao. Mkutano huo unapangwa kufanyika tarehe 7 hadi tarehe 8 Januari, na kufuatilia mipango ya ushirikiano wa kikanda hasa kuhusu pendekezo la amani la Hormuz lililotolewa na Iran mwezi Novemba kwenye Kikao cha 74 cha Baraza kuu la Umoja wa Mataifa. Maofisa wa kisiasa na wataalamu wa kanda hiyo wanatarajiwa kuhudhuria mkutano huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |