Rais Vladimir Putin wa Russia na mwenzake wa Marekani Donald Trump jana wamezumgumza kwa njia ya simu kuhusu ushirikiano katika mapambano dhidi ya ugaidi. Habari kutoka Kremlin zinasema idara ya ujasusi ya Marekani ilitoa habari kwa Russia hivi karibuni, ambayo ilisaidia Russia kuvunja njama ya shambulizi la kigaidi. Rais Putin amemshukuru Trump kutokana na tukio hilo. Habari zinasema idara ya usalama ya Russia tarehe 27 iliwakamata warussia wawili waliotaka kufanya shambulizi katika msimu wa sikukuu ya mwaka mpya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |