Mshambuliaji wa timu ya Simba Deo Kanda maesema bao alilofunga jumamosi dhidi ya KMC ni salamu kwa Yanga watakapokutana nayo Januari 4 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Kanda ambaye ni mchezaji wa timu ya TP MAzembe ya DRC na anachezea Simba kwa mkopo, amesema hana presha ya kucheza mchezo huo wa watani wa jadi. Katika msimu huu, Kanda ameifungia Simba mabao mawili, moja katika ligi dhidi ya KMC na bao jingine katika mchezo wa mashindano ya Kombe la FA dhidi ya AFC Arusha.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |