Wizara ya mambo ya nje ya Iraq imetangaza kumwita balozi wa Marekani nchini humo kuzungumzia shambulizi dhidi ya kambi ya kikosi cha taifa cha Iraq cha Hashd Shaabi, ambalo limesababisha vifo vya watu 25 na wengine 51 kujeruhiwa. Wizara hiyo imesema shambulizi hilo linalopaswa kulaaniwa, limeingilia uhuru wa Iraq. Iraq, ikiwa ni nchi huru, haitoruhusu nchi yake kuwa medani ya mapambano wala njia ya kushambulia nchi nyingine.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |