Jaji James Makau aliamuru kesi iliyowasilishwa na Cofek isikizwe Februari 17, 2020.
Jaji Makau alisema , kesi hiyo ingelisikizwa Januari 2020 lakini anasikiza kesi nyingine katika mahakama kuu pamoja na majaji wengine wawili zinazohusu masuala ya katiba.
Akiwasilisha kesi ya Cofek, wakili Henry Kurauka, ameeleza mahakama kwamba wakazi wa Nairobi hawakuarifiwa kama inavyotakiwa kisheria kabla ya kuongeza ada za magari ya wamiliki binafsi na ya kibiashara.
Ada ya kuegesha gari dogo iliongezwa kutoka Sh200 hadi Sh400.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |