• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Wenyeji wa Sewrengetiu wakatiwa umeme kwa deni la shilingi milioni 43

    (GMT+08:00) 2020-01-01 19:34:17
    Wakazi wa mji wa Mugumu wilayani Serengeti mkoani Mara nchini Tanzania wamelazimika kukaa bila umeme baada ya kukatiwa kufuatia deni la Sh43 milioni wanalodaiwa na shirika la Umeme Tanzania (Tanesco). Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mugumu (Muguwasa) imekuwa kwenye mgogoro wa muda mrefu na Tanesco kutokana na kulimbikiza madeni na kila mwezi wamekuwa wakikata umeme kushinikiza malipo na kusababisha ada kubwa kwa wananchi.

    Kaimu fundi mkuu wa Tanesco wilaya hiyo, Peter Mtete leo amesema kuwa malipo waliyoona kwenye mfumo ni Sh3 milioni, hivyo hawataweza kufungua huduma hadi deni lote litakapolipwa.

    Ameongeza kuwa wana wateja 1500 kati ya wakazi zaidi ya 35,000 wa mji huo ambao walikuwa wanawatoza Sh7,500 sawa na Sh11,250,000 kwa mwezi, umeme ni Sh9-10 milioni lakini wanashindwa kulipa hata kidogo, wamepandisha gharama hadi Sh12,000 kwa mtu mwenye matumizi madogo ambapo wanaweza kusanya Sh18 mil lakini hakuna mabadiliko.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako