Kipa wa Ajax Amsterdam Andre Onana ambaye ni raia wa Cameroon amesema makipa wenye asili ya Afrika hawana nafasi katika klabu kubwa kutokana na rangi. Kipa huyo mwenye miaka 23 amesema licha ya ubora wa makipa kutoka Afrika, lakini klabu kubwa haziwapi nafasi kwa sababuya ubaguzi. Ameweka wazi kuwa, mwaka 2017, klabu nyingi zilionyesha nia ya kumchukua, lakini baada ya mazungumzo aliambiwa kuwa mashabiki hawakubali makipa wanaotokea Afrika. Amesema mashabiki hawaamini kuwa kipa wa Afrika ana kiwango bora cha kucheza katika klabu kubwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |