Timothy Cheruiyot, nyota anayejitahidi kurithi mikoba ya Asbel Kiprop ambaye ni bingwa wa mbio za mita 1,500 aliyefungiwa kwa miaka minne kwa kutumia dawa za kuongeza nguvu, ametangaza kuwa mwaka huu utakuwa wa kukimbizana na rekodi ya dunia katika mita hizo. Mbio hizo huhusisha mizunguko mitatu na robo ya mita 400. Mwaka 1998 rekodi ya dunia ilivunjwa na Hicham Guerrouij wa Morocco aliyetumia sekunde 55 kwa kila mzunguko na kuweka rekodi mpya ya dakika 3:26 mjini Rome, Italia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |