• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kiongozi mkuu wa Iran aapa kulipiza kisasi kwa Marekani kufuatia mauaji ya kamanda wa kundi la IRGC

    (GMT+08:00) 2020-01-03 17:03:37

    Kiongozi mkuu wa Iran Ayatollah Ali Khamenei amesema, nchi hiyo itajibu vikali mauaji ya kamanda wa Kikosi cha Mapinduzi ya Kiislam (IRGC) Meja Jenerali Qassem Soleimani.

    Khamenei amesema lengo la Soleimani na harakazi zake za ukombozi hatitasimama kutokana na kifo chake, bali zitaendelea kwa nguvu zaidi, na ushindi dhahiri unawasubiri wale wanaopigana katika njia hiyo.

    IRGC leo imethibitisha kuwa, Meja Jenerali Soleimani ameuawa katika shambulizi la anga lililotokea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Baghdad.Kiongozi huyo ametangaza siku tatu za maombolezo kufuatia kifo cha Soleimani.

    Wakati huohuo, Wizara ya Ulinzi ya Marekani imesema, jeshi lake lilifanya shambulizi lililomuua kamanda huyo wa IRGC.

    Siku hiyo Wizara ya mambo ya nje ya China Bw. Geng Shuang amesisitiza kuwa China inapinga matumizi ya nguvu katika mahusiano ya kimataifa, na kuihimiza Marekani idumishe utulivu na kujizuiza.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako