• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya: Wafanyibiashara wadogo kulipa ushuru

    (GMT+08:00) 2020-01-03 17:19:49
    Katika hatua ya punde zaidi ambayo huenda ikazidisha mambo kuwa magumu kwa wananchi, serikali kuanzia jana ilianza rasmi kutoza ushuru wamiliki wa biashara ndogo ndogo kama vinyozi, mama mboga na sekta ya Juakali ushuru wa moja kwa moja.

    Ushuru huu unatozwa hata baada ya kuwa, tayari wananchi wanakabiliwa na hali ngumu za kiuchumi. Kuanzia Jumatatu, wazazi wanawarejesha watoto wao shuleni ambapo watahitajiwa kugharamikia sare, vitabu na hata karo kwa wanaosoma shule za kibinafsi, za upili na vyuoni.

    Sasa itakuwa lazima kwa kila mfanyibiashara mdogo kulipa ushuru wa asilimia tatu kwa mauzo ya kila mwaka.

    Kufikia mwishoni mwa mwaka jana, Kenya ilikuwa na deni la Sh6 trilioni kutoka mashirika mbalimbali ya kifedha ulimwenguni na ya humu nchini.

    Hii ina maana kuwa huenda bidhaa na huduma katika sekta ya jua kali zitapanda kutokana na ushuru huu mpya, unaotokana na sheria ya fedha ya 2019 ambayo Rais Uhuru Kenyatta aliidhinisha mwaka jana.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako