Ushuru huu unatozwa hata baada ya kuwa, tayari wananchi wanakabiliwa na hali ngumu za kiuchumi. Kuanzia Jumatatu, wazazi wanawarejesha watoto wao shuleni ambapo watahitajiwa kugharamikia sare, vitabu na hata karo kwa wanaosoma shule za kibinafsi, za upili na vyuoni.
Sasa itakuwa lazima kwa kila mfanyibiashara mdogo kulipa ushuru wa asilimia tatu kwa mauzo ya kila mwaka.
Kufikia mwishoni mwa mwaka jana, Kenya ilikuwa na deni la Sh6 trilioni kutoka mashirika mbalimbali ya kifedha ulimwenguni na ya humu nchini.
Hii ina maana kuwa huenda bidhaa na huduma katika sekta ya jua kali zitapanda kutokana na ushuru huu mpya, unaotokana na sheria ya fedha ya 2019 ambayo Rais Uhuru Kenyatta aliidhinisha mwaka jana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |