Mshauri wa kiongozi mkuu wa Iran kuhusu masuala ya ulinzi wa taifa Bw. Hossein Dehqan jana amesema, nchi hiyo itachukua hatua ya kijeshi dhidi ya Marekani kutokana na mauaji ya Meja Jenerali Qassem Soleimani, aliyekuwa kamanda wa kikosi cha Quds katika Jeshi la Mapinduzi ya Kiislamu la Iran.
Shirika la habari la Tasnim limemnukuu Dehqan akisema, Iran itachukua hatua ya kijeshi dhidi ya vituo vya kijeshi vya Marekani, huku akisisitiza kuwa Iran haitaki vita na Marekani, lakini ni lazima kulipiza kisasi kwa Marekani kwa pigo kubwa iliyoitoa kwa Iran.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |