• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Viongozi wa Ufaransa na Marekani wazungumza kwa njia ya simu kuhusu mvutano wa Mashariki ya Kati

    (GMT+08:00) 2020-01-06 08:48:22

    Taarifa iliyotolewa jana na Ikulu ya Ufaransa imesema, rais Emmanuel Macron siku hiyo alizungumza kwa njia ya simu na mwenzake wa Marekani Donald Trump kuhusu hali ya mvutano katika kanda ya Mashariki ya Kati.

    Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kwenye mazungumzo hayo rais Macron amesema Ufaransa inapenda kushirikiana kwa pamoja na pande mbalimbali za kikanda na kimataifa ili kupunguza mvutano wa sasa katika kanda ya Mashariki ya Kati, na kwamba muungano wa kimataifa unatakiwa kuheshimu kikamilifu mamlaka ya Iraq na kuendelea kutoa kipaumbele katika kupambana na kundi la kigaidi la IS, ili kuhakikisha usalama wa Iraq na utulivu wa kanda nzima.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako