Kutokana na hali ya wasiwasi inayozidi kuwa mbaya kwenye kanda ya Mashariki ya Kati, waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Heiko Maas, amesema Ujerumani imetoa pendekezo kwa mjumbe mwandamizi wa Umoja wa Ulaya anayeshughulikia sera za diplomasia na usalama na kushauri kuitisha mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya wiki hii, ili kufikia mapema maoni ya pamoja kuhusu kuchukua hatua za pamoja.
Ofisi ya chansela wa Ujerumani imetangaza kuwa chansela Angela Merkel atafanya ziara nchini Russia tarehe 11, kufanya mazungumzo na rais Vladimir Putin wa Russia kuhusu masuala mbalimbali yakiwemo Iraq na Iran.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |