Novak Djokovic ameiongoza Serbia katika robo fainali ya michuano ya tenisi ya kombe la ATP nchini Australia kwa kushinda mechi za mchezaji mmoja mmoja na wachezaji wawili wawili dhidi ya mahasimu wao Ufaransa. Baada ya Benoit Paire wa Ufaransa kumshinda Dusan Lajovic, Mchezaji namba mbili duniani Djokovic alimlaza chali Gael Monfils kwa 6-3 6-2. Djokovic na Viktor Troicki waliwashinda Nicolas Mahut na Edouard Roger-Vasselin kwa 6-3 6-7 (5-7) huko Brisbane Australia. Naye Rafael Nadal wa Hispania alimshinda mchezaji wa Uruguay na kukamilisha nane bora.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |