Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari ya Kenya, Daniel Manduku alisema msongamano wa umepunguza na kuwezesha shughuli kufanyika kwa haraka.
Alisema bandari hiyo ilishughulikia kakontena milioni 1.425 mnamo 2019 ikiwakilisha ukuaji wa asilimia 7.3 zaidi ya mwaka uliopita.
Bwana Manduku alisema usafirishaji wa haraka wa shehena kwa njia ya Reli kwenda kwa bandari kavu mjini Nairobi umetatua msongamano wa bandari na sasa wanatarajia kupeleka treni zaidi ya 10 kila siku.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |