Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran IRGC limeripotiwa kurusha "makumi ya makombora" dhidi ya Kituo cha jeshi la anga la Marekani cha Al-Asad nchini Iraq. Mpaka sasa hakuna ripoti kuhusu vifo na majeruhi kutokana na shambulizi hilo.
Wizara ya ulinzi ya Marekani imethibitisha kutokea kwa shambulizi hilo. Ikulu ya Marekani imesema rais Trump amearifiwa na kufuatilia kwa karibu maendeleo ya tukio hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |