Michuano ya SuperCup ya Hispania iliyopewa msukumo mpya inatarajiwa kuanza kutimua vumbi leo nchini Saudi Arabia, hatua ambayo itaongeza kipato kwa Shirikisho la Soka la Hispania. Hata hivyo, michuano hiyo imeyakasirisha makundi ya haki za binaadamu na mashabiki nchini humo. Real Madrid na Valencia zinakutana katika nusu fainali ya kwanza mjini Jeddah kabla ya Barcelona kupambana na Atletico Madrid kesho Alhamis. Mchezo wa fainali utafanyika siku ya Jumapili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |