Kocha wa timu ya Taifa ya soka ya wanawake chini ya umri wa miaka 17 nchini Tanzania, Bakari Shime, amesema anatarajia timu yake itafanya vizuri katika mashindano ya kufuzu Kombe la Dunia 2020 nchini India. Shime amesema, wanatarajia kucheza na Burundi Januari 12 katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, na kwamba maandalizi ya mchezo huo yanaendelea vizuri. Pia amesema wachezaji wake wote wako vizuri na hakuna majeruhi, na anachosubiri ni siku ya mchezo tu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |