Waziri wa ulinzi wa Marekani Mark Esper amesema katika shambulizi lililotokea jumanne, Iran ilirusha makombora 16 ya masafa mafupi kutoka sehemu tatu nchini Iran.
Bw Esper amesema makombora 11 kati ya 16 yamefikia kituo cha kijeshi cha Al-Asad na lisilopungua moja kufikia kituo kingine karibu na Erbil. Ameongeza kuwa makombora hayo yameharibu mahema, barabara za ndege, maegesho na helikopta moja.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |