Alisema kwa muda mrefu maeneo ya kihistoria yalikosa kufanyiwa ukarabati na kupelekea kukiosesha serikali mapato.
Akizungumza katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi vyumba vya kihistoria ya Wareno eneo la Fukuchani Mkoa wa Kaskazini Unguja ,Balozi Karume alisema maeneo ya kihistoria yanaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa kukuza uchumi wa nchi iwapo miundombinu yake itafanyiwa ukarabati na kuwa kivutio cha utalii.
Alisema serikali ya Dk.Ali Mohamed Shein imeweka mikakati ya kuyafanyia marekebisho maeneo ya kihistoria ili kuongeza idadi ya watalii wanaoingia nchini humo.
Aidha aliwaomba wananchi ,taasisi binafsi,shehia na wanafunzi kushirikiana na Idara ya Makumbusho na Mambo ya Kale katika kuyalinda na kuyatunza maeneo hayo ili yaweze kuwa endelevu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |