Kocha mpya wa Klabu ya Yanga, Luc Eymael raia wa Ubelgiji amewasili jijini Dar es Salaam na kuelekea Zanzibar jioni jana na kuungana na kikosi cha klabu hiyo inayoshiriki Michuano ya Kombe la Mapinduzi. Eymael, ametua jijini Dar es Salaam jana Alhamisi, Januari 9, 2019, na kuanza kazi rasmi baada ya kumaliza taratibu za vibali vya kufanya kazi nchini. Akizungumza mara baada ya kutua kwenye ardhi ya Bongo, Eymael amesema kuwa anaona fahari kujiunga na timu kubwa ndani ya Afrika. Ameongeza kuwa anaitambua vema falsafa yake na namna ilivyo hivyo ana imani atakwenda nayo sawa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |