Mtanzania Rashid Ramadhani ametwaa medali ya fedha katika mashindano ya Teniss Afrika Mashariki na Kati ambayo yanamalizika leo katika viwanja vya klabu ya Gymkhana jijini Dar es Salaam. Rashid alipoteza mchezo huo wa fainali dhidi ya Hakizumwami Junior wa Rwanda kwa seti 2 – 0 za 6 – 2 na 6 – 4. Rashid alianza viUri na kuonyesha utulivu mkubwa mwanzoni mwa mechi hiyo huku mpinzani wake akilalamika mara kwa mara kwa mwamuzi ambaye alilazimika kusimamisha mchezo na kumpa onyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |