Gavana wa Lamu, Fahim Twaha, Kamishna wa Kaunti hiyo Irungu Macharia na Kamanda wa Polisi eneo hilo, Muchangi Kioi, wamesema Lamu kwa sasa imedhibitiwa vilivyo kiusalama na kwamba wawekezaji, watalii na wanabiashara wengine wako huru kuzuru eneo hilo wakati wowote ili kuendeleza azma yao ya maendeleo.
Katika kikao cha jumla na wanahabari kwenye makao makuu ya Kaunti ya Lamu mjini Mokowe mnamo Jumatano, viongozi hao pia waliwataka wakazi eneo hilo kuondoa shaka na badala yake kuelekeza fikra zao katika kujiendeleza maishani.
Bw Twaha aliwashukuru walinda usalama kwa juhudi zao katika kuhakikisha amani na utulivu vinarejea eneo hilo.
Alisema serikali yake itaendelea kushirikiana kwa karibu na idara ya usalama ili kuona kwamba amani na utulivu vinadumishwa Lamu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |