Kaimu gavana wa benki kuu ya Sudan Badral-Din Abdel Rahim, amenukuliwa akisema kwamba benki kuu haitajihusisha tena na shughuli ya kuuza na kununua dhahabu. Juma lililopita, kampuni moja ya kibinafsi ilitumia fursa hii kuuza kilo 155 za dhahabu nje ya taifa la Sudan.
Serikali ya Sudan kupitia Wizara ya Hazina ya Kitaifa, imechukuwa hatua hii ili kukusanya pesa zaidi kuisaidia katika shughuli zake za kila siku, ikizingatiwa kwamba sasa, Sudan inakumbwa na wakati mgumu kiuchumi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |