Rais Xi Jinping wa China ametoa salamu za kumpongeza Haitham bin Tariq al-Said kwa kurithi usultani wa Oman. Amesema tangu kuanzishwa uhusiano wa kibalozi kati ya nchi hizo mbili, uhusiano wa pande mbili umepata maendeleo makubwa na pande hizo zimekuwa wenzi wa kimkakati wanaoaminiana. Rais Xi amesema anatilia mkazo juu ya maendeleo ya uhusiano kati ya China na Oman, na yuko tayari kushirikiana na sultani Haitham ili kuboresha uhusiano wa wenzi wa kimkakati wa nchi hizo kwenye ngazi mpya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |