Timu za mpira wa wavu wa ufukweni za Rwanda kwa upande wa akina dada zimejihakikishia tiketi ya kuingia raundi ya pili kwenye michuano ya kucheza Olimpiki ya Tokyo 2020 kufuatia ushindi dhidi ya Kenya na Uganda. Rwanda iliwakilishwa na timu mbili katika michuano hiyo ya siku tatu ya Sub-Zone 5 iliyofanyika Dar es Salaam, Tanzania, ambayo ilikamilka jana mchana. Baada ya raundi hiyo ya kwanza kukamilika, raundi ya pili itafanyika mwezi ujao. Timu zitakazofanya vizuri kwenye raundi ya pili zitafuzu kucheza michuano ya mabingwa ya Afrika inayofanyika Juni mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |