Bondia mkongwe nchini Tanzania, Rashid Matumla amesema bondia Salum Mtango ana kiwango kizuri na anaamini ana nafasi ya kutwaa mkanda wa ubingwa wa dunia wa UBO dhidi ya mpinzani wake Suriya Tatakhum wa Thailand. Mabondia hao wanatarajiwa kukutana katika pambano la raundi 10 uzani wa Light litakalofanyika Januari 31, mwaka huu kwenye uwanja wa Mkwakwani, jijini Tanga. Matumla amesema bondia wake alianza mazoezi mapema ili kujiandaa na pambano hilo na anaamini kuwa atapeperusha vizuri bendera ya Tanzania.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |