Mashindano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati maarufu kama Kombe la Kagame mwaka huu yamepangwa kufanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Klabu ya Simba ndio mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara na Yanga ambayo ilimaliza katika nafasi ya pili msimu uliopita zina nafasi ya kushiriki mashindano hayo. Katibu mkuu wa Baraza la Soka la Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) Nicholas Musonye amesema, uamuzi huo umepitishwa rasmi katika mkutano mkuu wa Baraza hilo uliofanyika Desemba mwaka jana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |