Rais Xi Jinping wa China amesisitiza kuwa, China inatakiwa kukuza mapambano dhidi ya ufisadi katika sekta ya fedha, kuongeza nguvu ya viwanda vya serikali katika kupambana na ufisadi, na kuimarisha usimamizi wa raslimali na mali za taifa.
Pia amesisitiza kuwa inapaswa kujenga na kuimarisha usimamizi wa vitendo vya udanganyifu kwenye mashirika ya matibabu, kukamilisha mfumo wa usimamizi wa mali za taifa ndani na nje ya nchi, na kuimarisha ukaguzi na usimamizi kwa maofisa wanaowajibika katika ngazi mbalimbali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |