Watu 21 wakiwemo watoto wanane na wanawake watano wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa kwenye mashambulizi makali ya anga yaliyotokea kaskazini magharibi mwa Syria wikiendi hii. Hata hivyo, makubaliano ya kusimamisha vita yaliyoanza kutekelezwa Jumapili yameripotiwa kuleta utulivu wa kiasi. Msemaji wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Stephane Dujarric amesema Umoja huo unazitaka pande zote na wale wenye ushawishi na pande hizo kulinda usalama wa raia na miundombinu ya kiraia, pamoja na majukumu yao kwa mujibu wa sheria ya ubinadamu ya kimataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |