• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Iran yawakamata baadhi ya watu kutokana na kuhusika na ajali ya ndege ya Ukraine

    (GMT+08:00) 2020-01-14 17:15:11

    Msemaji wa idara ya sheria ya Iran Gholamhossein Esmaili amesema, Iran imekamata baadhi ya watu kutokana na kuhusika kwao katika ajali ya ndege ya Ukraine iliyosababisha vifo vya watu 176 waliokuwa ndani ya ndege hiyo.

    Akizungumza na waandishi wa habari, Bw. Esmaili amesema mpaka sasa uchunguzi kuhusu wahusika umefanyika, na wataalamu wa sheria wanajitahidi kuhoji, kuchunguza na kukusanya taarifa.

    Amesema sanduku jeusi limepelekwa Ufaransa, na wataalamu wa Iran na Ukraine watashiriki kwenye kazi ya kusoma data.

    Jumamosi wiki iliyopita, jeshi la Iran lilisema, limeangusha kwa makosa ndege ya abiria ya Ukraine, na kosa hilo la kibinadamu linapaswa kulaumiwa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako