Bunge la Ukraine limetaka uchunguzi wa wazi, huru na kamili ufanywe dhidi ya ajali ya ndege ya abiria ya Ukraine iliyotunguliwa mjini Tehran Januari 8. Taarifa iliyotolewa na bunge hilo pia imewataka viongozi wa Iran kushirikiana vizuri na nchi za nje na mashirika ya kimataifa na kutoa msaada kadri iwezavyo kwenye uchunguzi huo. Bunge la Ukraine pia linaitaka Iran iombe msamaha rasmi na kukubali kuwajibika na ajali hiyo ya ndege.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |