Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepitisha azimio la kukuza bodi ya ushauri ya Kamati yake ya Utawala na Bajeti yaani Kamati ya Tano. Azimio hilo limeamua kuongeza idadi ya wajumbe wa Kamati ya Ushauri kuhusu Hoja za Utawala na Bajeti kutoka 16 hadi 21 kuanzia tarehe mosi, Januari mwakani. Azimio hilo limeteua viti vitano kwa makundi ya Afrika na Asia Pasifiki mtawalia, viti vinne kwa Latin Amerika, Caribbean na Ulaya Magharibi na sehemu nyingine mtawalia na vitatu kwa Ulaya Mashariki.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |