Somalia imezindua msako wa watuhumiwa watano wa ugaidi walioshiriki kwenye uhalifu wa kigaidi nchini humo.
Serikali ya Somalia imetangaza majina na picha za watuhumiwa hao na kuwataka raia watoe taarifa zitakazowezesha kukamatwa kwao. Serikali pia imetangaza donge nono kwa taarifa zozote zitakazosaidia kukamatwa kwa watuhumiwa hao.
Watuhumiwa wanne kati ya hao wamehukumiwa adhabu ya kifo kutokana na uhalifu wa kigaidi, na mwengine amehukumiwa kifungo cha maisha. Watu hao wanatuhumiwa kuwaua watu kadhaa nchini Somalia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |