Kamisheni ya Uchumi wa Afrika ya Umoja wa Mataifa ECA imesisitiza haja ya kuhimiza uvumbuzi wa kiteknolojia kwenye sekta ya fedha ili kubadilisha sura ya uchumi wa Afrika.
Mbali na wito huo ECA pia imesema ripoti mpya yake kuhusu Uchumi wa Afrika ERA-2020 ambayo inatarajiwa kutolewa mwezi Machi, itatathmini nafasi ya uvumbuzi wa kifedha na kiufundi katika mageuzi ya sekta ya biashara barani Afrika.
Kwa mujibu wa ECA ripoti hiyo itaangalia ujuzi uliopo kuhusu uvumbuzi wa kifedha, ikiwemo teknolojia za kifedha Fintech na jinsi mavumbuzi hayo yanavyoweza kuhimiza maendeleo ya sekta ya biashara barani Afrika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |