• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tamasha la kusherekekea mwaka mpya wa jadi wa kichina kufurahisha watazamaji

    (GMT+08:00) 2020-01-15 14:28:24

    Jaribio la kwanza la Tamasha la Mwaka 2020 la Sikukuu ya Mwaka Mpya wa Jadi wa Kichina limefanyika kwa mafanikio kwenye ukumbi No.1 wa Shirika Kuu la Utangazaji la China.

    Licha ya Beijing, tamasha hilo lenye maonesho ya ngonjera, nyimbo, ngoma, opera, viinimacho na sarakasi pia litakuwa na majukwaa mkoani Henan na katika sehemu ya ghuba kubwa ya Guangdong, Hong Kong na Macao.

    Kuanzia mwaka 1983, Shirika Kuu la Televisheni la China ambalo sasa liko chini ya Shirika Kuu la Utangazaji la China limekuwa likiandaa tamasha kila mwaka wakati wa mkesha wa sikukuu ya mwaka mpya wa jadi wa kichina, na tamasha hilo limekuwa kitu kisichokosekana kwa Wachina katika kusherehekea mwaka mpya.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako