• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Vipers yaongoza, KCCA yaona Nyota

    (GMT+08:00) 2020-01-15 16:28:04

    Timu ya Vipers FC ya Uganda imeendelea kuongoza Ligi Kuu ya StarTimes ya Uganda (SUPL) kwa kufikisha alama 42 baada ya kupata ushindi wa magoli 4 – 2 dhidi ya Proline katika mechi iliyochezwa jana jioni huko Lugogo. Kocha wa timu hiyo Edward Golola amewashukuru wachezaji wake kwa kufuata maelekezo yake na hivyo kujipatia ushindi huo. Katika mchezo mwingine uliochezwa Kavumba, timu ya Bright Stars iliendelea kuinua matumaini yake kwa kupata ushindi wa pili mfululizo katika raundi ya pili kwa kuifunga KCCA bao 2 – 1, hivyo kuondoa matumaini ya KCCA kuendelea kushikilia taji la Ligi hiyo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako