Mshikizi wa rekodi ya dunia kwa mbio za Marathon Eliud Kipchoge amesema analenga kutimiza kitu cha muhimu katika mbio za London Marathon zitakazofanyika April mwaka huu. Kipchoge, ambaye pia ataongoza timu ya wanariadha wa Kenya katika mashindano ya Olimpiki ya Tokyo baadaye mwaka huu, amesema sio tu kwamba anataka kushinda, bali kutimiza kitu kingine, ambacho labda ni kuvunja rekodi yake ya dunia ya kutumia 2:01:39 aliyoiweka katika mbio za Berlin Marathon mwaka 2018.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |