• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya: Wakuzaji wa India wajadili mpango wa kuwekeza kwenye sekta ya kahawa

    (GMT+08:00) 2020-01-16 19:34:11
    Wakulima wa kahawa katika kaunti ya Kirinyaga wanatarajiwa kupata faida iwapo ushirikiano kati ya serikali ya kaunti hiyo na wanunuzi kutoka India utafanikishwa.

    Gavana wa Kirinyaga Anne Waiguru ameanzisha mazungumzo kati ya serikali yake na wawekezaji wa India ambao wameelezea nia ya kununua kahawa.

    Vile vile, amekuwa akifanya mazungumzo na wasimamizi wa vyama 15 vya ushirika kutoka eneo la Mlima Kenya kwa lengo la kuimarisha bei ya zao.

    Wawekezaji hao kutoka India ambao ni wanachama wa kampuni ya SPG group of Companies, watarajiwa kuanza kununua kahawa baada ya makubaliano kuafikiwa.

    Gavana Waiguru alifafanua kuwa serikali yake itahakikisha wakulima wanauza kahawa yao kwa mkataba wa miaka 10 ambapo watahakikishiwa mapato ya kudumu.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako