Balozi wa Marekani nchini Kyle McCarter ametangaza kwamba serikali yake inaendelea kupunguza msaada wa kifedha kwa Kenya na badala yake kuhimiza ushirikiano wa kibiashara ili kufanikisha ukuaji wa kiuchumi.
Bw McCarter alisema anaamini Kenya ni taifa ambalo halifai kutegemea misaada na badala yake linafaa kuwa kielelezo bora kwa mengine kwenye ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
Kauli ya balozi huyo inajiri huku kukiwa na sintofahamu kwamba Marekani imepunguza ufadhili wake kwa miradi muhimu jambo ambalo limeathiri hali ya maisha ya raia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |