• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya: Marekani yaonelea bora kufanya biashara na Kenya badala ya misaada

    (GMT+08:00) 2020-01-16 19:35:05

    Balozi wa Marekani nchini Kyle McCarter ametangaza kwamba serikali yake inaendelea kupunguza msaada wa kifedha kwa Kenya na badala yake kuhimiza ushirikiano wa kibiashara ili kufanikisha ukuaji wa kiuchumi.

    Bw McCarter alisema anaamini Kenya ni taifa ambalo halifai kutegemea misaada na badala yake linafaa kuwa kielelezo bora kwa mengine kwenye ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

    Kauli ya balozi huyo inajiri huku kukiwa na sintofahamu kwamba Marekani imepunguza ufadhili wake kwa miradi muhimu jambo ambalo limeathiri hali ya maisha ya raia.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako