Mkuu wa idara ya sera ya fedha ya Benki kuu ya China Bw. Sun Guofeng, amesema kuongezeka hivi karibuni kwa kiwango cha ubadilishaji wa fedha za RMB kunahusiana na makubaliano ya awali ya uchumi na biashara kati ya China na Marekani, huku athari zake zikiendelea kudumu.
Bw. Sun amesema kusainiwa kwa makubaliano hayo kunanufaisha China, Marekani na dunia nzima, ambako pia kunainua imani ya soko la dunia likiwemo la China. Soko la sarafu za kigeni na masoko mengine ya fedha pia yamekuwa na mwitikio, na matokeo chanya ya hatua hiyo yataendelea kudumu.
Tangu mwezi Agosti mwaka jana, kiwango cha ubadilishaji wa RMB kwa dola za kimarekani kinaendelea kupanda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |