Wizara ya biashara ya China imesema, thamani ya kandarasi ya huduma ya China katika mwezi Januari hadi Novemba mwaka 2019 imeongezeka kwa asilimia 11.4, na inatarajiwa kufikia dola za kimarekani bilioni 95.
Mkurugenzi wa idara ya biashara ya huduma katika wizara ya biashara ya China Bw. Xian Guoyi amesema, thamani ya biashara ya huduma ya China nchini Marekani, mkoa wa Hongkong, Umoja wa Ulaya na Japan imeongezeka na kuchukua nafasi nne za mwanzo za masoko makuu duniani.
Pia idadi ya mikataba iliyotolewa na makampuni ya China katika nchi na sehemu za "Ukanda Mmoja, Njia Moja" pia imeongezeka.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |