Makampuni ya mafuta hurejesha gharama zao ndani ya miaka kadhaa baada ya uzalishaji na uuzaji wa bidhaa hiyo unapoanza ,huku bei za chini za mafuta zikiashiria kiwango cha chini cha kurejesha gharama za uwekezaji.
Bei za mafuta ghafi zimekuwa chini ya $75 kwa pipa tangu mwezi Oktoba,2018,huku Tullow ikiangalia bei za sasa za bidhaa hiyo kama msingi wa bajeti yake.
Kampuni hiyo imetumia zaidi ya $1 bilioni katika uchimbaji na utafutaji mafuta nchini Kenya pekee ,na haikubainika wazi ni kiasi gani kimefutwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |