Ofisa wa Idara ya afya ya Yemen amesema jeshi la serikali ya nchi hiyo lilishambuliwa kwa makombora na kundi la Houthi kwenye kituo cha jeshi kilichoko mkoani Marib, hadi sasa askari zaidi ya 80 wameuawa na wengine 150 wamejeruhiwa vibaya. Rais Abdrabbuh Mansur Hadi wa nchi hiyo ametoa taarifa akilaani kundi la Houthi kutokuwa na "udhati wa kutafuta amani", akiliamrisha jeshi la serikali likae tahadhari ya ngazi ya juu, ili kukabiliana na hali ya dharura.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |