• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rais Vladimir Putin wa Russia ateua mawaziri wapya wa Baraza la mawaziri

    (GMT+08:00) 2020-01-22 09:23:38

    Ikulu ya Russia imetangaza amri kupitia tovuti yake kuwa, rais Vladimir Putin wa Russia amewateua mawaziri wapya.

    Kwa mujibu wa amri hiyo, serikali mpya itapunguza idadi ya manaibu waziri wakuu kutoka 10 hadi 9. Msaidizi wa zamani wa Ikulu Kremlin Andrey Belousov kuwa naibu waziri mkuu wa kwanza. Yury Borisov, Yury Trutnev na Tatyana Golikova wataendelea kuwa manaibu mawaziri wakuu. Dmitry Grigorenko ameteuliwa kuwa naibu waziri mkuu mpya. Kutokana na amri nyingine, Sergei Lavrov pia ataendelea kushika wadhifa wake wa waziri wa mambo ya nje.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako