Mkuu wa Shirika la nishati ya atomiki la Iran(AEOI)Bw. Ali Akbar Salehi amezilaumu Uingereza, Ufaransa na Ujerumani kwa kuanzisha utaratibu wa mzozo kwenye makubaliano ya suala la nyuklia la Iran.
Amesema kitendo hicho kimetokana na shinikizo na madai ya Marekani, na kimethibitisha ukosefu wa uwezo wa Ulaya wa kukabiliana na madai ya Marekani.
Habari zinasema, wiki iliyopita, nchi hizo tatu zilitangaza kuchukua hatua kuanzisha utaratibu wa mzozo na Iran.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |