Shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji duniani IOM limesema limewarejesha nchini Sudan kwa usalama wahamiaji haramu 129 kwa hiari yao kutoka Libya. Shirika hilo limesema kutokana na mpango wa pamoja wa Umoja wa Ulaya na IOM, wahamiaji hao watapokea msaada wa kuendesha maisha yao. IOM inatekeleza mpango wa kuwarejesha wahamiaji haramu kwa hiari yao wanaohamishwa kutoka Libya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |