Shirika la afya duniani WHO jana usiku lilifanya mazungumzo ya dharura kuhusu kama maambukizi ya virusi vipya vya nimonia aina ya 2019-nCoV nchini China yamekuwa tukio la dharura la afya ya umma ya kimataifa PHEIC.
Mkurugenzi mkuu wa WHO Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema kwenye mkutano na waandishi wa habari, kuwa yalikuwa majadiliano mazuri, lakini ni dhahiri kwamba taarifa zaidi zinahiajika. Hivyo shirika hilo limeamua kufanya mkutano tena leo. Amesema anazingatia sana kuhusu kutangaza au la kama maambukizi hayo ni tukio la dharura la afya ya umma ya kimataifa, na atatoa uamuzi huo kwa kuzingatia ushahidi wote.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |