Rais Abdel Fattah al Sisi wa Misri amekutana na maofisa waandamizi wa nchi hiyo kujadili bwawa la GERD la Ethiopia lililojengwa kwenye mto wa Nile unaochangiwa na Misri, Ethiopia na Sudan.
Msemaji wa rais wa Misri Bw. Bassam Rady amesema waziri mkuu, mawaziri wa ulinzi, mambo ya nje na rasilimali ya maji, na mkuu wa idara ya ujasusi wamehudhuria mkutano huo. Rais Al-Sisi ameelezea msimamo wa Misri katika mazungumzo hayo kwa kuzingatia msaada wa Marekani kwa mazungumzo hayo ya pande tatu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |