• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Mahakama nchini Tanzania yawafungia wavuvi wanane kwa miaka mitatu kwa uvui haramu

    (GMT+08:00) 2020-01-23 19:21:06

    Mahakama ya Wilaya ya Chato nchini Tanzania imewahukumu kifungo cha miaka mitatu jela wavuvi wanane kila mmoja baada ya kuwakuta na kosa la kufanya uvuvi isivyo halali katika hifadi ya taifa ya Burigi-Chato iliyoko kaskazini magharibi mwa nchi hiyo, baada ya wavuvi hao kushindwa kulipa faini.

    Mahakama hiyo pia imekamata injini tatu za boti na boti moja ya uvuvi ambayo wavuvi hao waliitumia kwa uvuvi haramu, na kuamuru kuchomwa kwa neti zao.

    Januari 19 mwaka huu, mamlaka nchini Tanzania zilitangaza msako maalum dhidi ya watu wanaoingiza vifaa haramu vya uvuvi, na kusema kitendo hicho kimeathiri sekta ya uvuvi nchini humo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako